
BENDI
ya muziki wa dansi ya Msondo, wasanii nyota wa Bongo Fleva, H. Baba,
Nay wa Mitego na Stamina wanatarajia kulipamba Bonanza la Jogging la
Global Breaking News 15778 litakalofanyika katika Ukumbi wa Dar Live,
Mbagala-Zakhem, jijini Dar, Februari 9 mwaka huu.

Mratibu wa Bonanza hilo, Rajabu Mteta (KP) ameiambia Mikito Nusunusu
kuwa kabla ya wasanii hao kupanda jukwaani kuanzia asubuhi hadi jioni,
kutakuwa na jogging (mbio za taratibu) zitakazosimamiwa na wenyeji, Kejo
Jogging Sports Club, kuanzia uwanja wa taifa majira ya saa 12 na nusu
hadi ukumbini Dar Live.…
BENDI
ya muziki wa dansi ya Msondo, wasanii nyota wa Bongo Fleva, H. Baba,
Nay wa Mitego na Stamina wanatarajia kulipamba Bonanza la Jogging la
Global Breaking News 15778 litakalofanyika katika Ukumbi wa Dar Live,
Mbagala-Zakhem, jijini Dar, Februari 9 mwaka huu.

Mratibu
wa Bonanza hilo, Rajabu Mteta (KP) ameiambia Mikito Nusunusu kuwa
kabla ya wasanii hao kupanda jukwaani kuanzia asubuhi hadi jioni,
kutakuwa na jogging (mbio za taratibu) zitakazosimamiwa na wenyeji, Kejo
Jogging Sports Club, kuanzia uwanja wa taifa majira ya saa 12 na nusu
hadi ukumbini Dar Live.

Alisema
zaidi ya klabu 200 kutoka wilaya zote za mkoa wa Dar es Salaam
zimethibitisha kushiriki matembezi hayo huku klabu kadhaa za soka,
netiboli, darts na pool table zikishindana katika bonanza hilo kwa
kiingilio cha shilingi 2000 kwa wasio wanamichezo.
Mteta alizitaja klabu za soka zitakazopepetana kwenye tamasha hilo
kuwa ni veteran kutoka Taifa, Hamasa, Buguruni, Mwembechai, Azam,
Oilcom, Machava, Ufukoni, Dovia, Scud, Mafaza, Sakaramento, Kejo, Police
Baracks, Magereza, Temeke, Uamsho, Mjengo na Global.
Pia alizitaja timu zitakazochuana katika mchezo wa netiboli kuwa ni
Hamasa, Barracks, Buguruni, Kejo, Mwembechai, New Habari 2006 Ltd, The
Golden, Ndiyo sisi Netiboli, Classic, Global na Magenge 20.
Pia
kutakuwa na michezo mingine kama kuvuta kamba, bao la kete, drafti,
karate, kukimbia na gunia, ngumi na michezo maalum ya watoto ambayo
itaambatana na zawadi.
Meneja wa Kampuni ya Global Publishers ambao ndiyo wanaotoa huduma ya
Global Breaking News, Abdallah Mrisho, amesema kupitia bonanza hilo,
wataitambulisha huduma hiyo mpya inayowezesha wasomaji wanaotumia
mtandao wa Vodacom kupata habari mbalimbali za papo kwa hapo katika simu
za mkononi.
“Tutaizindua rasmi huduma ya Global Breaking News ukumbini. Kwa
wanaotaka kujiunga na huduma hii, wataandika neno Global katika uwanja
wa meseji kisha kutuma kwenda namba 15778, burudani Bongo Fleva na bendi
ya Msondo kama kawa,” alisema Mrisho.
No comments:
Post a Comment