POOL PARTY

POOL PARTY

Wednesday, February 26, 2014

Baada ya kuhairishwa Valentine Day,uzinduzi wa USIKU WA KIGODORO kufanyika Jumamosi hii,Dar Live

Ile filamu ya Kigodoro ambayo ilihairishwa uzinduzi wake siku ya Valentine mwezi huu,sasa kufanyika Jumamosi hii pande za Dar Live,Mbagala.Muandaaji wa uzinduzi huo,Zamaradi Mketema amesema kwa kushirikiana na Global Publishers walihairisha uzinduzi huo ili kuufanya uwe na burudani za kutosha na kuwapa mashabiki kitu cha uhakika.Alisema kuwa katika uzinduzi huo wa Usiku wa Kigodoro watakuwepo wasanii mbalimbali kama Msagasumu a.k.a Mkali wa Kigodoro, Rihama Ally,Shamsha Ford,Wema Sepetu,Kajala Masanja na wengineo.
Naye Staa wa filamu za Kibongo,Wema Sepetu amesema kuwa hajawahi kuhudhuria Kigodoro na ana hamu sana ya kukiona na na kuwaambia mashabiki wajitokeze kwa wingi Jumamosi hii

No comments:

Post a Comment