POOL PARTY

POOL PARTY

Friday, February 28, 2014

HEMED ACHUKIA KUITWA TOZI

Stori: Brighton Masalu
MSANII wa filamu na Bongo Fleva, Hemed Suleiman ‘PHD’ amefunguka kuwa anachukizwa na tabia ya watu kumwita tozi au mtu wa maringo.
Hemed Suleiman ‘PHD’.
Hapa anafafanua: “Wananihukumu kwa macho, mimi siyo tozi ila usafi wangu na kutoonekana mara kwa mara kunanifanya nionekana hivyo lakini kiuhalisia siko hivyo.”

WEMA SEPETU AKIRI KUNENEPA SABABU YUPO KIMAPENZI NA MTU AMPENDAYE KULIKO WOTE


Jana katika Kipindi cha leo Tena Mwanadada Wema Sepetu Aliulizwa kwanini Siku hizi ananenepa sana kiumbo na Mwanadada huyo mrembo alijibu moja kwa moja kuwa ananenepa kwa sababu ana amani ya moyo kwa vile yupo na mtu kimapenzi ampendaye kuliko wote duniani...Nadhani wote mnamjua ni nani?  Mapenzi raha Bwana asikwambie mtu ukimpata akupendaye na wewe anakupenda lazima unenepe

KAMA ULIKUWA HUJUI BASI HEMEDY PHD NA NAJMA SASA NG'ARE NG'ARE



Nimekutana na hizi picha za Hemedy akimbusu msanii wa muziki na filamu Najma na maneno yalioambatana na picha hizo yakizungumzia ndoa na harusi....Huenda sasa hawa ni mambo safi ...Najma alikuwa ni mpenzi wa Mr Blue zamani ......

SAKATA LA MGAGA WA DIAMOND: MKE WA MWENYE GARI LILILOIBWA AIBUKA, AFUNGUKA

Stori:  Sifael Paul
Lile sakata la kukamatwa kwa yule mganga wa staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’, Ustadh Yahya kwa msala wa wizi wa gari, limechukua sura mpya baada ya mke wa mwenye gari, Edric Magayane kuibuka na kufunguka mazito.
Mganga wa staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’, Ustadh Yahya.
Akizungumza na gazeti hili, mke huyo aliyejitambulisha kwa jina la Emida Denson alisema kuwa gari hilo aina ya Toyota Rav4 lilikuwa mali ya familia kabla ya mumewe kudai lilipata ajali hivyo lipo gereji.
Alisema kuwa baadaye mumewe alidai kuwa aliliuza akaongezea fedha kisha akanunua lingine aina ya Toyota Prado.
Alisema habari kuwa gari hilo liliibwa maeneo ya Kariakoo-Msimbazi, Dar hazikuwa za kweli kwani ukweli ni kwamba mumewe huyo alikuwa amemhonga mwanamke aliyemtaja kwa jina moja la Mwanahamis.
“Huyo Mwanahamis amenisababishia mateso makubwa kwenye ndoa yangu karibia miaka miwili sasa. Yaani ndoa yangu ni sarakasi tupu kwa sababu yake.
Edric Magayane na mkewe Emida Denson.
“Ukweli ni kwamba baada ya kuhongwa lile gari alikuwa hajui kuliendesha. Alichokifanya akamwachia Ustadh. Hayo mengine ya kushirikiana juu ya biashara zao za uganga hayanihusu.
“Sasa basi baada ya kuona gari liko mikononi mwa Ustadh ndipo mume wangu akalitaka ndiyo maana wamefikia hapo.
“Kinachoniuma ni kwamba mbali na gari, mume wangu alifikia hatua ya kuja kumpangishia Mwanahamis jirani na nyumba yetu maeneo ya Machimbo-Mwisho wa Lami (Yombo jijini Dar)
“Mbaya zaidi watu wakawa wanamuona mume wangu akiingia kwa Mwanahamis, nimedhalilika sana.
“Nalea watoto wanne peke yangu, wakwangu wawili na wawili wa mume wangu kwa mwanamke mwingine.
Staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’.
“Baada ya kuona ndoa inanitesa nilikwenda kwa mchungaji Kimaro aliyefungisha ndoa yetu kwenye Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Usharika wa Kariakoo nikamweleza mateso ninayopata.
“Alituita wote, akasemwa lakini baada ya hapo manyanyaso yakaendelea japo walihamia Banana-Ukonga ndiko wanakoishi hadi leo.
“Pia nilikwenda kwenye Dawati la Jinsia wilayani Temeke na baadaye Ustawi wa Jamii.
“Huko kote ilishindikana na sasa bora anipe talaka yangu tugawane mali kwa sababu nilipokutana naye hakuwa na kitu chochote, tulikuwa tukilala chini,” alisema mwanamke huyo kwa uchungu huku akitoa cheti cha ndoa (nakala ipo).
Kwa upande wake mume wa mwanamke alipotafutwa na kusomewa mlolongo wa sarakasi alizozieleza mkewe, alisema kuwa gari hilo lilikuwa mali yake na kwamba lilipata ajali likakaa gereji muda mrefu na lilipopona alikuwa akilitumia mwenyewe.
Kuhusu kuwa na hawara Mwanahamis, jamaa huyo alidai kwamba aliamua kuwa na mwanamke huyo kwa kuwa mkewe alikuwa ana matatizo ambayo hata hivyo hakutaka kuyaainisha.
“Naishi naye (mkewe) lakini kila mtu na chumba chake, huyo mwanamke ana matatizo yake ndiyo maana nikatafuta mtu mwingine, hizo habari anazolalamika, anazusha tu, nimempa uhuru aniache na wangu na yeye atafute mwanaume mwingine,” alisema mwanaume huyo.
Kuhusu gari analodaiwa kukutwa nalo mganga wa Diamond, habari zilieleza kuwa Ustadh aliachiwa kwa dhamana na bado gari hilo lipo mikononi mwa polisi likisubiri kesi kwenda mahakamani.

MASKINI AFANDE SELE

Stori:  Erick Evarist na Joseph Shaluwa
SIKU chache baada ya kuzagaa kwa taarifa za kuachana na mkewe mama Tunda, mfalme wa Rhymes, Seleman Msindi ‘Afande Sele’ ameibuka na kusimulia mambo ya kusikitisha waliyopita katika safari ya maisha yao.
Mfalme wa Rhymes, Seleman Msindi ‘Afande Sele’.
Akizungumza na wanahabari wetu ndani ya Ukumbi wa Meeda, Sinza-Mori, Dar, juzi Afande alisema hadi kufikia hatua ya yeye kutangaza kuwa ameachana na mama Tunda ambaye amedumu naye kama mume na mke kwa zaidi ya miaka 10, alikuwa akivumilia mambo mengi na mwisho kuamua kuachia ngazi.

Afande Sele akiwa na familia yake.
“Nilikuwa nikielezwa mengi kuhusu mke wangu, nilishapigiwa simu na kuambiwa mke wangu anagombaniwa na wanaume usiku klabu lakini huwa mimi siyo mtu wa kuishi kwa hisia, nilivumilia nikiamini atajirekebisha, haikuwa hivyo.
“Japo sikuwa na uthibitisho wa moja kwa moja, lakini nyumbani alikuwa siyo mtu wa kutulia, amekuwa akinizunguka hadi kwa washkaji zangu wa karibu. Kuna jamaa alichoshwa na habari hizo akanifuata na kuniambia hata kama lakini uvumilivu wangu ulizidi,” alisema Afande kwa hisia.
Akiendelea kushusha masikitiko yake mbele ya kinasa sauti cha Risasi Jumamosi, Afande alienda mbele zaidi kwa kusema mbali na mkewe huyo kumsaliti kwa wanaume tofauti wakiwema marafiki zake, ilifika wakati mama Tunda akawa anachukua fedha ndani na kwenda kutumia na wanaume.
Alisema alitumia mwanya wa mkali huyo wa mashairi anapokuwa amesafiri katika shoo mbalimbali na kuachiwa fedha za matumizi pamoja na ujenzi wa nyumba yao mpya, kutanulia.
“We acha tu, yaani fedha za matumizi, ujenzi nilikuwa namuachia lakini cha kusikitisha ni kwamba alizitumia kutanulia, jambo ambalo nililizidi kunitia umaskini na machungu ukizingatia jamii inaniheshimu kama msanii, mbaya zaidi wananchi wamenitaka nigombee ubunge Morogoro Mjini,” alisema Afande.
Akizidi kushusha ‘vesi’, Afande alitiririka kuwa kuna wakati aliwahi kupewa taarifa na rafiki yake mwingine aishie Kurasini jijini Dar ambaye alilamika juu ya mkewe kufika kwa jamaa huyo na kuazima fedha bila kuzilipa.
Kwenye aya nyingine, mkali huyo alisema anakumbuka jinsi alivyoishi na familia yake, mkewe, wanaye Tunda na Ahsante Sanaa lakini hana jinsi kwani ameona bora kuachana kwani umri wake una mruhusu kuoa mke mwingine siku ikitokea.
“Nakumbuka maisha kidogo ya furaha na familia, mama Tunda atabaki kuwa mama wa watoto wangu lakini kamwe hawezi kurudi kwangu kwani itakuwa ni aibu juu ya aibu,” alisema.
Afande aliachana na mama Tunda mwishoni mwa mwaka jana alipotimba jijini Dar katika shughuli zake za kikazi na kumuachia mkewe fedha za ujenzi lakini aliporejea nyumbani Morogoro, alikuta mzazi mwenzake huyo ameondoka nyumbani na kuacha funguo, kila alipompigia simu hakupokea.
Alipoulizwa kuhusiana na shutuma zilizoporomoshwa na Afande, mama Tunda alitiririka:
“Alinipa Sh. milioni 3 za shoo tu, tukanunua vifaa vya ujenzi lakini siyo kwamba nilitanua na wanaume, tena kama ni kumfumania, mimi ndiye nilimkuta na mwanamke alitoka naye Fiesta Dodoma, sikutaka tu kumsema, hizo taarifa anazusha tu.
“Kwanza kuna mambo mengi tu amenifanyia, alikuwa mlevi kwani hadi wazazi wangu walikuwa wakinishangaa sana, sasa na mimi nikaona bora niachane naye,” alisema mama Tunda.

AMANDA NA GONJWA LISILOELEWEKA

Stori: Gladness Mallya
STAA wa sinema za Kibongo, Tamrina Posh ‘Amanda’ amepatwa na ugonjwa wa ajabu  ambao haujulikani.
Staa wa sinema za Kibongo, Tamrina Posh ‘Amanda’.
Katika mazungumzo na paparazi wetu, Amanda alisema: “Naumwa sana na nimechukua vipimo vingi ikiwemo malaria na presha pale Agha Khan (hospitali) lakini hakijagundulika chochote ingawa mwili wote unauma.”

WEMA SEPETU"NAPENDA WANAUME WEUSI NA NI KWELI NIPO NA DIAMOND"


Mwanadada Wema Sepetu ambaye pia aliwahi kuwa Miss Tanzania 2006 ambaye kwa sasa anaendesha kampuni yake binafsi iitwayo Endless Fame inayojishughulisha zaidi na utengenezaji wa Filamu mbalimbali.

Kupitia kipindi cha Leo tena February 28 Wema Sepetu amekubali kutaja sifa za mwanaume anayempenda kuwa na mvuto kwake,swali lililoulizwa na Watangazaji wa kipindi hicho ni kuhusu mwanaume wa sifa gani anayedhani anaweza kuolewa nae ambapo Wema alijibu “Kuolewa sio shida je huyo mwanaume nampenda,maana naweza kuja kuchumbiwa lakini nisimpende”


“Mimi nampenda Mwanaume mweusi,wanaume weupe sio kwamba sijawahi kuwa nao lakini nakuwa sina mzuka nao”.
Alipoulizwa kuhusu uhusiano wake na Diamond amekiri kwa kusema’Kweli niko na Nasib - Diamond na nadhani muda huu kutakua na utulivu ndani yake,ule utoto tuliokua tunafanya nadhani ulikua utoto na imekua Power Couple toka mwaka 2010 kwa hiyo tuna ni miaka 4 sasa,kwa sasa tumeamua kuwa serious’.

Habari kwa Hisani ya Millard Ayo

Wema Sepetu pia kaandamana na Ant Ezekiel kwenye interview ya kipindi hicho kinachorushwa na Clouds Fm.

WASTARA: NINAHITAJI KUPUMZIKA, KUJIFUNGIA


Stori: Brighton Masalu
STAA wa kike mwenye uwezo wa kucheza na hisia kwenye filamu za Kibongo, Wastara Juma, amesema kwa sasa anahitaji muda mwingi wa kupumzika kutokana na misukusuko mingi iliyomkumba siku za hivi karibuni.
Wastara Juma.

Akiteta na paparazi wetu kwa sauti ya chini na ya upole alisema: “Nahitaji muda mwingi wa kupumzika jamani, kuna mambo yameniondoa kabisa kwenye ‘mudi’ ya kawaida hivyo natumia muda mwingi kuwa peke yangu.”

WABUNGE WAWALIPUA BONGO MOVIES WASEMA NI OMBA OMBA BALAA


SKENDO nzito ya Bongo Muvi imeibuliwa na baadhi ya wabunge waliopo mjini Dodoma kufuatia kuwalipua wasanii wake kuwa, ni ombaomba balaa, Risasi Jumamosi lina mkanda mzima.

Kwa mujibu wa wabunge hao ambao walitaka majina yao yasitiriwe kwa sasa, baadhi ya wasanii hao ambao wengi ni mastaa wamekuwa wakiwazukia na kuwapiga mizinga jambo linalowashangaza hasa wakizingatia kuwa, wapiga mizinga hao wana majina makubwa na huonekana wakitembelea magari ya kifahari.

“Hivi nyie mapaparazi, mnashindwa kabisa kukomesha hii tabia ya mastaa wa Bongo Muvi? Hawa jamaa ni ombaomba sana.

“Wamekuwa wakitupiga mizinga sana. Tunawashangaa maana wengine wana majina makubwa, wanatembelea magari ya kifahari lakini bado wanaomba pesa ndogo,” alisema mbunge mmoja ambaye anatoka kwenye moja ya majimbo ya Mkoa wa Dar es Salaam.

KINACHOWASHANGAZA WABUNGE
Kwa mujibu wa wabunge hao, linalowashangaza zaidi ni kwamba wasanii hao ambao  ni wake kwa waume, wamekuwa wakipiga mizinga ya pesa ndogo badala ya kuomba pesa za kufanyia mambo makubwa yenye mikakati mizito.

“Mtu anakuja, anasema anasumbuliwa na kodi ya nyumba au anasema hajala. Hivi kweli mastaa wakubwa kama akina…(anataja jina) ni wa kuomba vijisenti kama vya kodi ya nyumba jamani?” alihoji mbunge mwingine kati ya watano waliokuwa wakizungumza na gazeti hili.

Waheshimiwa hao waliendelea kuwaanika mastaa hao kwa kudai kwamba, walichogundua ni kuwa inapotokea wakapewa hitaji lao la fedha, huishia kukaa baa hadi usiku wa manane na asubuhi wakiamka wako vilevile kama hawakupewa.

MWAKIFWAMBA ABANWA NA RISASI
Ili kuweka sawa madai hayo mazito na yenye aibu kubwa kwa tasnia hiyo maarufu nchini, Risasi Jumamosi lilimtafuta Rais wa Shirikisho la Filamu Tanzania ‘TAFF’, Simon Mwakifwamba ambaye alikiri kuwepo kwa malalamiko hayo ya wasanii wake kuwa ombaomba!

HUYU HAPA MWAKIFWAMBA
“Ni kweli kabisa. Mimi mwenyewe nimewahi kusikia malalamiko hayo, lakini unajua tena ni mambo binafsi, mtu anapiga mizinga kwa mambo binafsi si rahisi kumwingilia,” alisema rais huyo.
Aliendelea kusema kuwa, katika vikao mbalimbali vya kisanii, amewahi kuweka wazi msimamo wa taasisi kwamba kila msanii aishi maisha yenye heshima huku akiwa mbali na mazingira yenye kusababisha aibu katika jamii.

KUMBE HATA JK ALIWAHI KUMLALAMIKIA
Katika kuonesha hasira zake juu ya tuhuma hizo zenye dharau katika gemu la filamu, Mwakifwamba alikwenda mbele zaidi kwa kusema kuwa, katika moja ya mazungumzo yake na Rais wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Kikwete ‘JK’ aliwahi kumlalamikia kwamba, wapo mastaa ambao kazi yao ni kupiga mizinga isiyo na tija.

“Rais mwenyewe aliwahi kuniambia kuna wasanii wakiwasiliana na yeye wanamwambia mambo ya pesa za kula.

“Kuna msanii aliwahi kumtumia meseji JK akimwambia, ‘mjukuu wako leo hali mbaya’,” alisema Mwakifwamba.
Akaendelea: “Sasa we’ unakutana na rais badala ya kumweleza mikakati mikubwa na nini cha kusaidiwa kuifanya tasnia iweze kuendelea, unapiga mizinga hujala, ni aibu sana.”

WALISHAMPIGA ‘MIZINGA’ HADI ‘MTOTO WA MKULIMA’
Mwakifwamba hakukubali kufumba midomo yake bila kupasua yote ambapo alizidi kudai kuwa, hawashangai sana wasanii wake hao kwani waliwahi kumpiga mizinga hadi Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Mizengo Kayanza Peter Pinda ‘Mtoto wa Mkulima’. 
“Niliwahi kukutana na Waziri Mkuu Pinda, nikamwomba mambo ya kuisaidia tasnia ya filamu Tanzania, akasema afadhali mimi nimeongea vitu vya maana, kuna wenzangu alikutana nao ‘wakambomu’ fedha za matumizi binafsi, nilishangaa sana,” alisema Mwakifwamba. 

RISASI LAWASAKA MASTAA, WAPATIKANA HAWA:
Jacqueline Wolper, ni staa wa filamu za Kibongo. Filamu yake ya kwanza ni Ama Zao Ama Zangu. Yeye alipoulizwa kuhusu madai hayo, alisema:
“Ni kweli, sikatai kwamba hiyo tabia ipo tena sana tu. Lakini wanaoongoza ni mastaa wa kiume, hao ndiyo wanaotutia aibu ya kuonekana sisi ni o
mbaomba.”

STEVE NYERERE
Yeye ndiye Mwenyekiti wa Bongo Movie Unity. Alisema anavyojua kuna kuonana kirafiki na waheshimiwa na kuonana kiajenda.
“Tabia ya kuomba fedha kwa waheshimiwa ipo. Lakini linapokuja suala la tasnia yetu kupeleka hoja kwao, tunaanza hoja baada ya hapo kuna waheshimiwa wengi wana urafiki na wasanii, tunaitana pembeni na kupiga kirungu.
“Siwezi kukaa na waheshimiwa kama Rostam Aziz, William Ngeleja, Mheshimiwa Abood na Nimrod Mkono halafu nikawaacha hivihivi, kisa eti mimi ni Mwenyekiti wa Bongo Muvi,” alisema Steve akionesha kumshangaa mwandishi aliyempigia simu kutaka usawa wa mizani ya habari hiyo. 
ODAMA YEYE
Jennifer Kyaka ‘Odama’ yeye alipata umaarufu mkubwa kupitia Tamthiliya ya Odama iliyokuwa ikirushwa na Televisheni ya Taifa (wakati huo TVT). Alipopigiwa simu iliita kwa muda mrefu bila kupokelewa licha ya kurudiwa mara kadhaa.
AUNT EZEKIEL
Risasi pia lilimtafuta  nyota mwingine aliye mahiri kwenye sinema za Bongo, Aunt Ezekiel ambaye filamu iliyompaisha sana inaitwa Miss Tanzania. Yeye simu yake ya mkononi ilionesha kutokuwa hata na laini kwa wakati huo.

RAY AFUNGUKA
Staa mkongwe katika gemu tangu enzi za Kaole Sanaa Group, Vincent Kigosi ‘Ray’ aliposakwa na kuulizwa kuhusu madai hayo ya wasanii kuwa ombaomba alisema:
“Wasanii wengi wanawaza maisha ya hapa na si baadaye. Badala ya mtu kuweka shida zake kwenye mfuko wa karatasi, anaweka kwenye rambo ambao unapiga kelele.
“Mwisho wa siku anaomba shilingi milioni tatu akagombolee gari au asaidiwe kodi ya nyumba, anasahau kuwa kapata nafasi ya kuonana na mheshimiwa azungumzie tasnia tunavyonyonywa hadi kuuza hati miliki,” alisem Ray.

SHARAPOVA, MWENZAKE WAMMIMINIA MABUSU NYAMWELE

Stori: Mwandishi Wetu MAHABA? Mnenguaji grade one Bongo, Asha Sharapova na mwenzake, Titi Mwinyi wamenaswa wakimmiminia mabusu motomoto, mnenguaji mwenzao wa Bendi ya Extra Bongo, Super Nyamwela.
Mnenguaji mpya wa Bendi ya Extra Bongo ‘Wazee wa Kizigo’, Asha Said ‘Sharapova’.
Tukio hilo lililogusa hisia za ‘wataalam wa mambo’, lilitokea hivi karibuni pande za Sinza-Afrika Sana jijini Dar. Nyamwela alipoulizwa kuhusiana na ishu hiyo, alisema ni ishara ya upendo wa kawaida na hakuna cha ziada.

Licha ya picha zinazosemekana kumdhalilisha kusambaa mitandaoni PNC aingia studio na Ostaz Juma na ku-record wimbo wa pamoja

Licha ya wadau na mashabiki wa sanaa kukasirishwa na video, audio pamoja na picha  iliyokuwa ikimuonyesha PNC akimpigia magoti Ostaz Juma na musoma akimuomba msamaha na kuomba kurudi katika kundi la Mtanashati linalosimamiwa na Ostaz, huku wakidai kuwa ni kumdhalilisha, PNC ameonekana kutokujali na kutamka wazi kuwa ataendelea kuwa mtanashati na wameshakubaliana na msamaha wake umekubaliwa.
Picha hiyo ya juu inamuonyesha Ostaz na PNC wakiwa ndani ya studio za Mazoo. Inasemekana wanarecord wimbo wa pamoja utakaoitwa "Thamani yangu"

Hizi ndio mpicha za Beyonce ambazo team yake ya PR itatamani kuziondoa haraka kwenye mitandao










Video: Mr. Blue, Dyna, Barnaba Boy na Amini warekodi wimbo wa kampeni ya dereva makini 2014





Ni ukweli usiopingika kuwa ajali zimekuwa ni mwiba mchungu kwa familia, jamii na taifa kwa ujumla unaoacha kilio, walemavu, yatima, wajane na wagane kila kukicha.
Katika kuunga mkono jitihada za kupunguza ajali barabarani wakali katika muziki wa bongo fleva Mr Blue, Amini, Barnaba Boy na Dyna Nyange wameshiriki kurekodi wimbo wao utakaotumika kwenye kampeni ya dereva makini inayolenga kuhamasisha uzingatiaji wa usalama barabarani na kwenye vyombo vya usafiri. Wimbo huo umerekodiwa na mtayarishaji wa muziki C9.

Kampeni hiyo ya dereva makini imeandaliwa na Transevents Marketing kwa lengo la kutoa hamasa kwa madereva kuwa makini wanapoendesha magari ili kuwawezesha abiria kufika salama waendako.
Audio ya wimbo wa dereva makini imesharekodiwa na kinachosubiriwa ni video yake, tazama video ya maelezo ukitumia link hii hapa chini.

STEVE NYERERE AMWAGIA SIFA LULU

Stori: Mayasa Mariwata
RAIS wa Bongo Movie Unit, Steven Mengere ‘Steve Nyerere’ amemmwagia sifa staa wa filamu Bongo, Elizabeth Michael ‘Lulu’ kuwa ni binti mdogo lakini sasa anajitambua tofauti na wasanii wengine wakubwa.

Elizabeth Michael ‘Lulu’.
Akipiga stori na Ijumaa Steve alisema kuwa, mbali na umakini katika kazi zake za kisanii, sasa hivi yuko makini sana na maisha yake kiasi kwamba ni nadra sana kumkuta na skendo za kijingajinga.
Steve Nyerere.
“Achilia mbali hao mastaa wote unaowajua wewe, mimi nikiwa kama kiongozi wa Bongo Movie siwezi kusema uongo, namkubali sana Lulu kwani ni binti mdogo na anajitambua na sasa siyo mtu wa kuendekeza mambo ya starehe kama wengine, pia huwezi kumuona viwanja kirahisi, katulia anafanya kazi,” alisema rais huyo.

USTAADH JUMA NA MUSOMA AFUNGUKA KUHUSU PICHA INAYOONEKANA KUWA NI YA KIDHALILISHAJI KWA MSANII PNC

Tangu jana usiku kuna picha ilikua imesambaa ikimwonyesha Msanii Pancras Ndaki a.k.a ‘PNC’ akiwa amempigia magoti boss wake wa zamani Ustadh Juma na Musoma, kama anamwomba msamaha na Ustadh ameonekana akiwa amekalia kochi huku amekunja nne, picha imekua gumzo.255 ya xxl ya clouds fm imepiga stori na Ustadh huyu hapa anafunguka kuhusu picha hii
Ikumbukwe kwamba Ustadh Juma alikua ana label, na ilikua na list ndefu ya wasanii kama Kitale, Dogo Janja, Sharomilionea, Suma Mnazaleti na wengine wengi, alipotemana na wasanii hao ndiyo akaamua kuimba yeye mwenyewe, anajiita Birdman wa Bongo.

AKON ASAIDIA BARA LA AFRIKA KWA KUSAMBAZA UMEME KWA MAKAZI ZAIDI YA MILL.1

Si kuamua tu kuongelea suala la kumiliki mke zaidi ya mmoja, kama vile King Mswati.
Staa wa muziki wa Kimataifa,Akon kutoka pande za Senegal ameamua kuligeukia Bara la Afrika na kutoa msaada unaostahili akishirikiana na makampuni yaliyojitolea katika kampeni hiyo iitwayo Akon Lighting Africa.Kwenye mradi wa mazingira wa kusambaza umeme kwenye makazi ya watu barani Afrika.
Inasemekana kwamba mradi huo ambao umekadiriwa kwamba mpaka itakapofika 2015 makazi zaidi ya million 1 barani Afrika yatakuwa yamepatiwa umeme kupitia mradi huo wa kusambaza umeme wa sola.
Tayari ameshatembelea nchi zaidi ya nne kwa ajili ya mradi huo ikiwemo Senegal, Mali, Guinea na Burkina Faso.

PNC AFUNGUKA BAADA YA KUPIGWA PICHA YA UDHALILISHAJI NA USTADHI JUMA NA MUSOMA

Kufuatia picha na video inayomwonyesha Msanii PNC akiwa amempigia magoti Boss wake wa zamani CEO wa mtanashati Ustaadh Juma na musoma, lawama nyingi zimemwangukia Ustaadh kwa kuziweka picha hizo mtandaoni
Siku ya jana PNC hakuweza kupatikana ila leo 255 ya xxl ya clouds fm imepiga naye stori.

KITALE ANUNUA UGOMVI WA PNC BAADA YA KUDHALILISHWA NA USTAADH JUMA NA MUSOMA

Msanii wa Comedy Kitale ameamua kununua ugomvi wa msanii wa Bongo Fleva,PNC na Ustaadh Juma na Musoma baada ya kumdhalilisha msanii huyo kwa kumrekodi video na kumpiga picha na kuzisambaza mtandaoni.Baada kuziona picha hizo Kitale aliamua kumpigia simu Ustaadh Juma na kuuliza kwanini ameamua kufanya kitendo hicho cha kidhalilishaji ambapo Ustaadhi Juma alimjibu mbovu.
Zaidi msikilize Kitale akitiririka.

WAKALI WA SONG LA CHELEWA,NAVY KENZO KUANGUSHA BONGE LA SHOO,MAISHA CLUB JUMAPILI HII

Navy Kenzo chini ya Nah Reel na Aika Jumapili hii watakua na show pande za Maisha Club.
Pia kutakuwa shindano la kudance ambapo litaendeshwa kuwatafuta watu watatu wanakaoweza kwenda sawa na Bokodo Dance na watu hao watatu watashiriki kwenye video ya Chelewa.

MIKE TEE"WASANII TUKIKAA KIMYA KWA HILO LA USTAZ JUMA TUTAKUJA VULIWA NGUO HADHARANI"


Msanii mwenzangu PNC kadhalilishwa sana na OSTADH JUMA kwenye MEDIA zote, me toka jana natafakari sana kwa mtu mzima kufanya kitendo kama kile, upande wangu nimeumia na nimeona kama mimi nimefanyiwa kitendo kile.
Sasa basi wasanii wenzangu, washabiki wetu , viongozi wa ngazi mbalimbali tunajua mambo haya yapo lakini yana kipimo, tukikaa kimya wako watakaotuvua nguo hadharani kisa sisi wasanii ambao tunadharaurika hatuna elimu hatuna kipato ila tunatumika na wachache kupata wanachotaka,
Je tufanye nini me nimeshindwa cha kufanya we need your support wenye uchungu wa muziki wetu na wasanii wa TANZANIA kwa ujumla

Thursday, February 27, 2014

ALI KIBA AELEZEA SABABU ZA UKIMYA WAKE KWENYE GAME YA MUSIC


Kwa kipindi kirefu mkali wa ‘Single Boy’ Ali Kiba amekuwa kimya bila kutoa kazi yake binafsi huku ukimya wake ukizua maswali mengi kwa mashabiki na wadau wa muziki Tanzania.

Lakini leo (February 25) Ali Kiba amezua maswali mengine kwa mashabiki wake baada ya kuweka kwenye Instagram picha inayomuonesha akiwa na AY na Mwana Fa na kuandika ‘@Aytanzania&007#mj record #wait for it bonge ya wimbo.’

Hata hivyo hakuweka wazi kama ni wimbo wake au ameshirikishwa na maswaiba hao.

Tovuti ya Times Fm imefanya mahojiano na Ali Kiba ambaye ameyajibu maswali hayo yote, maswali ambayo hapo awali yalikuwa na majibu ya kuhisia tu bila kuwa na uhakika.

Ali Kiba ameiambia tovuti hii kuwa aliweka picha hiyo kwenye Instagram lakini hakuweka maelezo ya kutosha kwa makusudi.

“Sababu ya kuweka vile ni katika kutaka tu kuwa-surprise watu kwa sababu sikupenda kuwambia ni ngoma ya nani ila nimewajulisha kuwa nimefanya nao na tumefanya kwa MJ, hiyo yote ni kutaka kuwa-surprise.” Amesema Ali Kiba.

Mwimbaji huyo amedai kuwa hadi sasa wimbo huo haujajulikana ni wa nani kati yake yeye, Mwana Fa na AY, “tumefanya wote…haijajulikana ngoma ni ya nani.”

Ali Kiba ameongeza kuwa mashabiki wampe miezi miwili ijayo na kisha watapata maelezo ya kutosha kutoka kwake na kwamba baada ya muda huo kila kitu kitakuwa sawa.

Mwimbaji huyo wa ‘My Everything’ ameeleza pia sababu za yeye kuwa kimya, pamoja na mpango wake kwa mwaka 2014 ambapo amedai kuwa ataachia albam yake mpya.

“Sababu ya kuwa kimya ni kumpush Abdu Kiba aweze kuwa sawa sawa na vilevile mimi ni mzazi kwa hiyo niko busy na jinsi ya kuwa baba. Yaani vitu vingi vyote nilikuwa nikifanya, wakati muda wote niliokuwa nikifanya hivyo vitu nilikuwa najiandaa na albam yangu nyingine ambayo ni ujio mpya…nakuja na everything.

“Albam ipo kwa sababu itakuwa chini ya usimamizi wa kampuni ambayo inanihost, na ndio maana nikakwambia nipe miezi miwili na watu watajua kila kitu kinachoendelea…itafanyika na usimamizi mzuri tu na process zote zitakuwa ziko okay. Ila siwezi kukwambia ntafanya na distributor gani lakini, wasimamizi wangu watafanya hilo, wasimamizi ambao wamenichukua ndio maana ukaona kimya kingi, ni ku-fight maandalizi na kumaliza ngoma.”

Wednesday, February 26, 2014

Baada ya kuhairishwa Valentine Day,uzinduzi wa USIKU WA KIGODORO kufanyika Jumamosi hii,Dar Live

Ile filamu ya Kigodoro ambayo ilihairishwa uzinduzi wake siku ya Valentine mwezi huu,sasa kufanyika Jumamosi hii pande za Dar Live,Mbagala.Muandaaji wa uzinduzi huo,Zamaradi Mketema amesema kwa kushirikiana na Global Publishers walihairisha uzinduzi huo ili kuufanya uwe na burudani za kutosha na kuwapa mashabiki kitu cha uhakika.Alisema kuwa katika uzinduzi huo wa Usiku wa Kigodoro watakuwepo wasanii mbalimbali kama Msagasumu a.k.a Mkali wa Kigodoro, Rihama Ally,Shamsha Ford,Wema Sepetu,Kajala Masanja na wengineo.
Naye Staa wa filamu za Kibongo,Wema Sepetu amesema kuwa hajawahi kuhudhuria Kigodoro na ana hamu sana ya kukiona na na kuwaambia mashabiki wajitokeze kwa wingi Jumamosi hii