POOL PARTY

POOL PARTY

Friday, November 29, 2013

TANZANIA, CONGO NA BURUNDI WAUNDA MUUNGANO WAO BAADA YA KUTENGENGWA


Wakati Kenya, Rwanda na Uganda zimeunda umoja unaoitwa `Umoja wa Walio Tayari’ , Tanzania, Burundi na Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo (DRC) nazo zimeanzisha ushirikiano baina yao.
  
Katika siku za karibuni kumekuwa na mtikisiko ndani ya Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) baada ya Tanzania na Burundi kutengwa na wenzao wa Kenya, Rwanda na Uganda katika baadhi ya masuala muhimu ya ushirikiano hasa wa kiuchumi.

Tanzania, Burundi na DRC nazo zimekutana ikiwa ni utekelezaji wa ahadi ya Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta ambaye aliliambia Bunge lililopita kuwa Tanzania inafikiria kushirikiana na nchi hizo.
Mkutano wa ujirani mwema
Akizungumza na waandishi wa habari baada ya mkutano wa Ujirani Mwema uliofanyika mjini Bujumbura, Burundi jana, Sitta alisema Tanzania, Burundi na Kongo zimekubaliana kuendeleza miundombinu ya barabara, reli, anga na usafiri wa maji katika Ziwa Tanganyika.
Alisema mkutano huo ulilenga kuboresha miundombinu ya usafiri katika Ziwa Tanganyika ambalo linaziunganisha Burundi Tanzania, DRC na Zambia.
Pia tumepanga kuendeleza reli ya kati kutoka eneo la Uvinza, Tanzania hadi Msongati, Burundi na pia kuunganisha Barabara ya Manyoni - Tabora - Kigoma kupitia Bujumbura hadi Kivu ya Kusini, DRC,” alisema Sitta.
Mkutano huo ulihudhuriwa na Sitta pamoja na Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki wa Burundi, Leontine Nzeyimana na Waziri wa Uchukuzi wa DRC, Jack Lukeba.
Pia tulitembelea Bandari ya Kalindo iliyoko katika Ziwa Tanganyika upande wa Burundi kwani tunataka kuboresha bandari za ziwa hilo,” alisema Sitta.
Waziri huyo alisema Tanzania na Burundi zitaunganishwa na Barabara ya Manyoni – Tabora - Kigoma na Barabara ya Manyovu - Mgina, Mabanda - Bujumbura itakayounganishwa mpaka Kivu ya Kusini, DRC.
Kuhusu usafiri wa anga, Sitta alisema nchi hizo zinaangalia uwezekano wa kuanzisha safari za ndege za Dar es Salaam mpaka Bujumbura.

DIAMOND "PICHA ZA ZOEZI LA KUWAFANYIA INTERVIEW WALE WALIOTUMA MAOMBI YA KAZI"




Siku ya jana tulifanya zoezi la kuwafanyia interview
 baadhi ya watu waliotuma maombi yao kwa
 mujibu wa ,tangazo la kazi nilillolitoa
                                                                      juzi,mwitikio
 wa watu ulikuwa mkubwa,watu waliotuma
 email zao pamoja simu,kiasi ilituwia vigumu 
kuwataka wote waje kwenye interview,ilitubidi
 tuchague baadhi ya watu ambao tulihisi wanaweza
 kukidhi sifa tulizozihitaji ingawa nao pia tulipata
 changamoto ya wengi wao kuja pasipo kuzingatia maelekezo 
 na maagizo ya tangazo lilivyotaka,hivyo jana 
nikishilikiana na wataalamu wa hizo sekta tulisaili
 na mwisho wa siku tutachukua wale wenye viwango
 tunavyovihitaji na kuungana na team ya WCB-WASAFI,.

CHIDI BENZ AMEVURUGWA KWELI..!! TAZAMA ALICHOKIONGEA KATIKA HII POST YAKE


Hakuna tena kitu kizuri kwa Chidi Benz siku hizi. Kwa muda mrefu rapper huyo ambaye hivi karibuni ametokea kukubalika sana nchini Kenya (thanks kwa mashavu anayopewa na Nonini) ameonekana kutoa yake ya rohoni yanayomuumiza kupitia Twitter.

Yeye na Wakazi kuna tatizo?
Picha lilianza jana, baada ya Wakazi kutweet: Na ningependa kusema pia AY, Dimpoz, Ally Kiba, FidQ, Shaa, Cpwaa, Black Rhino, Remi Ongala, Profesa Jay & Lady Jaydee ni other Local heros!
Baada ya kuona ujumbe huo wa Wakazi, Chidi alimuuliza kishari ‘nini?’
Wakazi alichuna. Chidi akaamua kuandika: Hujui kuongea huwezi muoga..unaweza kuandika hapa twitter. Nyie ndio mkianza kushindwa mnasifia maadui.#umal** tuu.”
Ujumbe huo ulivuta hisia za watu wengi akiwemo Madee aliyeuliza: Rasheeed nani tena kazingua?  Chidi alijibu:Mazafanta wanahisi wanajua kuliko wewe wakati mwenyewe saa zingine unaona hujijui..2
Hata hivyo hatuwezi kuthibitisha kama maneno hayo yalikuwa yakimlenga Wakazi ama mtu mwingine kwakuwa kabla ya hapo tayari alikuwa ameanza kuandika tweets za hasira.
“Game ilipo now na propaganda zake inaua vitu vingi tu.sisi tunaonekana tunalalamika ujinga but hatuna maisha mabaya. Viongozi wa nchi sio lazima mdil na bongo freva..haiongezi wewe kufatwa but unatuongezea uadui usio na lazima. Mi natangazwa kwa ubaya tuuuuu.ila nina marafiki bado na wengi wanaongezeka hata hapa.#nakaza roho,” aliandika Chidi.
Kunani?

RAY NA CHUCHU HANS SASA LIVE LIVE..WAOMBA WASIINGILIWE PENZI LAO



Stori: Gladness Mallya
AMA kweli penzi ni kikohozi kulificha huwezi! Hatimaye uliokuwa uhusiano wa chini kwa chini wa nyota wawili wa sinema za Kibongo, Vincent Kigosi ‘Ray’ na Chuchu Hans, siyo siri tena baada ya wahusika hao wakuu kujiachia ‘live’, Ijumaa limeshiba.

KIMAHABA ZAIDI
Ishu hiyo ilitokea mapema wiki hii ambapo Chuchu alitundika picha kwenye ukurasa wake wa Instagram akiwa na Ray chumbani kimahaba.
Kufuatia tukio hilo kuliibuka gumzo kubwa na kulifanya jambo hilo kuwa ndiyo habari ya mjini katika ulimwengu wa mastaa wa filamu za Kibongo.

Katika picha hiyo, Chuchu anayetumia jina la Chukichuku kwenye Instagram aliambatanisha na maneno yaliyosomeka ‘Me n U’ akimaanisha yeye na Ray hivyo kutoa fursa kwa mashabiki wao kusema chochote.
Kwa mujibu wa mashabiki hao, Ray na Chuchu kwa sasa ndiyo love bird au ‘maua’ yanayopendezesha tasnia hiyo.
“Mmependezaaa…mapenzi waziwazi,” ilisomeka komenti ya mmoja wa mashabiki hao.

“Nilikuwa simuelewi Ray lakini hapa nimemsoma. Wamependeza sana,” ilisomeka komenti nyingine iliyoungwa mkono na mashabiki wengi kwa kupata ‘likes’ nyingi.
Mwingine aliandika: “Sasa walichokuwa wanagombea Mainda (Ruth Suka) na Johari (Blandina Chagula) kipo wapi? Ona sasa wamekosa wote… hahahaaa… wawaache miaka isiyohesabika.”

HAKUNA KIFICHO TENA
Katika kunogesha mambo, baadaye Chuchu aliweka picha ya Ray akimsifia jambo lililodhihirisha kuwa kwa sasa hawafanyi tena kificho kama miezi kadhaa iliyopita.
Habari za chini ya kapeti kutoka kwa wasanii wenzao wanaokuwa nao lokesheni zilieleza kuwa wawili hao wamekuwa wakionesha waziwazi kuwa wao ni item (kitu kimoja).

“Kuna siku tulikuwa tuna-shoot maeneo ya Sinza-Mori (Dar), yaani ungewaona wala usingeuliza maana kama hujui kusoma, ungeangalia hata picha. Yaani mapenzi kama njiwa!
“Sasa hivi ndiyo uhusiano ambao upo ‘hoti’ kwenye tasnia yetu, sema ndiyo hivyo wenyewe walikuwa hawapendi ijulikane lakini naona wameshindwa kuendelea kujificha,” alisema mwigizaji huyo kwa sharti la kutotajwa gazetini.

CHUCHU ATAKA WASIINGILIWE
Baada ya kujikusanyia data, Ijumaa lilimtafuta Chuchu akiwa mmoja wa wahusika wakuu ambapo alipopatikana alikuwa na haya ya kusema: “Hayo ni mambo yetu binafsi, naomba tusiingiliwe katika mambo yetu.”
Ijumaa: Chuchu wewe ni kioo cha jamii na mashabiki wako wanataka kujua ukweli juu ya uhusiano wako na Ray. Unalizungumziaje hilo?

Chuchu: Weweee…sikia! Nimeshasema sitaki mtu aniingilie mambo yangu. Kwani mnataka nini nyiye?
Ijumaa: Je, hiyo picha mliyopiga chumbani ni hotelini au nyumbani?
Chuchu: Siwezi kukuelezea tumepiga wapi, iwe hotelini au nyumbani haiwahusu, naomba mniache jamani mbona hivyo? Kwani vipi? (kisha akakata simu).

KAKA MKUBWA VIPI?
Jitihada za kumpata Ray ‘Kaka Mkubwa’ katika tasnia ya filamu za Kibongo ili kupata neno lake juu ya ishu hiyo ziligonga mwamba baada ya simu yake ya kiganjani kuita bila kupokelewa na hata alipofuatwa ofisini kwake, RJ Productions pale Sinza-Mori, Dar hakupatikana.

KABLA YA PICHA
Kwa muda mrefu kumekuwa na madai mazito kuwa Ray na Chuchu wanatoka lakini habari hizo zilikosa mashiko kwa kuwa hakukuwa na ushahidi wowote.
Ilidaiwa kuwa hata ile vita ya hivi karibuni ambapo Johari na Chuchu walizichapa kavukavu ilitokana na kugombea penzi la Ray.

JOHARI ASARENDA
Hata hivyo, baadaye Johari alinyoosha mikono kuashiria ‘kusarenda’ na kumwachia Chuchu atawale ulingo ambao ulimshinda pia Mainda.
Ilidaiwa kuwa katika kutekeleza kile walichokiita mpango wa siri, Chuchu na Ray waliunda kampuni yao na kuipa jina la kolabo la Chura wakimaanisha Chuchu na Ray.

TATIZO KUBWA
Wakati hayo yakiendelea, taarifa rasmi ni kwamba bado Chuchu ni mke wa ndoa wa bosi wa Kampuni ya 2 Eyez Productions, Frank Mtao anayeishi ughaibuni huko Australia akiwa ni mwenyekiti wa Wabongo waishio pande hizo.

Mbali na kuwa mke wa mtu, pia Chuchu ni mama wa watoto wawili hivyo uhusiano wake tata na Ray unalenga kuzalisha tatizo kubwa kwenye ndoa ya Chuchu ikiwa ni miezi kadhaa tangu wawili hao walipodaiwa kufumaniwa na mwanaume mwingine wa Chuchu.

SOGANGE YUPO DAR..AJIFICHA KUKWEPA MAPAPARAZI



VIDEO Queen wa Bongo, Agnes Gerald Waya ‘Masogange’ ambaye alipata soo la kukamatwa na malighafi haramu aina ya Ephedrine Julai 5, mwaka huu nchini Afrika Kusini amejaa tele jijini Dar es Salaam, Ijumaa limethibitisha.
Masogange akipozi na Jack Patrick.
Masogange ambaye siku ya tukio alikuwa na nduguye, Melisa Edward baada ya kunaswa na madawa hayo kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Oliver Tambo uliopo Kempton Park jijini Johannesburg nchini humo alihukumiwa kwenda jela miezi 32 au kulipa faini ya shilinghi milioni 4.8 ambapo aliweza kulipa na kuwa huru.
Tangu aachiwe huru, Septemba mwaka huu, msanii huyo akawa hajulikani alipo huku baadhi ya ‘posti’ zake kwenye mtandao wa kijamii wa Instagram zikionesha yupo Tanzania au Afrika Kusini.
Masogange akipozi dukani Bongo.
Jumatatu iliyopita, mida ya saa kumi jioni, paparazi wetu alipigiwa simu na msomaji wa gazeti hili (jina tunalo) akisema amemwona Masogange akiingia kwenye duka la nguo lililopo Sinza Kamanyola, Dar akiwa peke yake.
Paparazi wetu alijipanga kwa kamera na kutia timu kwenye duka hilo ambapo hata hivyo muuzaji alisema aliondoka baada ya kufanya manunuzi ya kawaida.
Jumatano, Masogange alitumbukiza picha kwenye mtandao wake akiwa ndani ya duka hilo na modo maarufu nchini, Jacqueline Patrick.
Jack alipigiwa simu ambapo alikiri kuwa na Masogange siku ya Jumanne kwenye duka hilo. Akasema: “Mimi nilimkuta pale, tukapiga picha tukaachana, basi.”
Kwa kutumia namba yake ya simu ya mkononi, Masogange alipatikana na kukiri yupo Dar lakini akasema hakutaka kuweka wazi kwa sababu anawaogopa sana mapaparazi.

HIZI NDIZO SABABU 10 ZA WANAWAKE KUTOKUOLEWA NA KUISHIIA KUSAGANA TU


Pamoja na kuwa kuna wanawake husita kuolewa, lakini jambo hili si kubwa sana kwa wanawake kama ilivyo kwa wanaume.


 Kwa kiasi kikubwa katika suala la kutaka kuingia ndani ya ndoa, wanawake ni wengi ambao hutaka kufunga ndoa kuliko ilivyo kwa wanaume. Hilo tunaliona wazi tokana na shamra shamra awazo nazo mwanamke wakati wa maandalizi ya shughuli za Ndoa na Harusi.


Hata hivyo, kwa wale wanawake wachache ambao husuasua kuolewa hizi ni baadhi ya sababu zinazopelekea kusuasua huko. (Izingatiwe hii ni kwa wanawake ambao hawajawahi kuolewa kabisa)

 

Vigezo vilivyopitiliza viwango (hasa kwa muonekano)

 

Wanawake wengi hasa wa umri mdogo (lakini unatosha kuolewa) hutumia muda mwingi katika kuchagua aina ya mwanaume ambaye angependa awe mume wake.Wanawake hawa hujiamini zaidi na kusimamia sifa zile ambazo huamini ni muhimu mwanaume wa kumuoa awe nazo.  


Vigezo hivyo huwa hata kwa misingi ya muonekano wa mwanaume huyo – kuna wale ambao hutaka mwanaume huyo wa kumuoa awe na sifa kama vile, mrefu, aliyejazia kifua, mtanashati, sauti nzuri n.k. 


Inaweza kuwa kama mzaha na ikaonekana ni kipengele kidogo sana lakini bado kuna wale ambao anaweza kuwa tayari kuolewa ila hataki sababu tu huyo mwanaume hafananii vile ambavyo yeye anataka mumewe awe.

 

Kutaka mwanaume tajiri

 

Kuna wanawake ambao tayari wameshajiwekea akilini kuwa hatakubali kuolewa na mwanaume yeyote yule ambaye hana pesa nyingi.


 Yupo tayari kuolewa ila si kwa mwanaume mwenye uwezo wa kawaida – hata ikitokea mwanaume ana uwezo kidogo wa kuweza kujitosheleza, yeye bado huona huyo mwanaume hamfai hadi pale tu atakapo pata yule ambaye anahisi ataishi maisha ya kifahari.


 Hivyo hukazana kusubiri na kujitahidi kuwinda aina ya mwanaume ambaye atakuwa na uwezo mkubwa, bila kujalisha kama huyo mwanaume kampita sana umri.


 

Kutompata Mwanaume Ampendae

 

Hili ni kama tu vile ilivyo kwa wanaume ambao huamini ndoa haiwezekani na haifai bali tu hadi pale umpatapo yule ambaye unampenda na unaamini anakupenda pia.  


Wengi katika kundi hili huamini kuwa mafanikio ya ndoa kigezo kikubwa ni kupendana tu na mengine hufuata kwenye sababu ya upendo. Kunawanawake vigezo vya mwanamme awe vipi havina umuhimu kabisa katika kutaka kuamua kuolewa.


 Yeye kikubwa anataka ampate mume ambaye atampenda kwa dhati na huku akiwa na matumaini kuwa huyo mume atampenda na yeye pia kwa dhati.  Huyu mwanamke anaamini msingi bora wa ndoa ni mapenzi ya dhati kati ya yeye na mmewe basi! Hana haraka hadi pale atakapompata mwanaume akampenda ndipo atakapokuwa tayari kuolewa.  

 

Kuchagua mno Wanaume wa Kumuoa (SO SELECTIVE)

 

Kuna wale wachache ambao akili hubadilika kama kinyonga; wasioridhika wala kujitambua ni nini wanataka ama mwanaume wa aina ipi wanataka. 


Akija wa mwenye uwezo atasema nataka wa kuchuma nae, akija asiye na uwezo atatoa sababu tu hata kama kumlaumu kuwa inaonyesha hajitumi kutafuta maendeleo. 


Akija wa kabila hii, atasema hapana hao wana tabia hii mimi siitaki! Yaani kwa ufupi ni mtu asiyeisha kutoa kasoro za wale ambao wanajitokeza kutaka kumuoa.


 Hatimaye inaweza tokea muda wa kuolewa ukapita na akaishia kupunguza uchunguzaji lakini ikiwa hata wanaume wa umri wa kufaa kumuoa kutokuwepo tena katika soko.

 

Kujiona ni mzuri sana

 

Kuna wanawake ambao ni kweli Mwenyezi Mungu kawajaalia uzuri hasa (uzuri wa muonekano), anakuwa ni mzuri kiasi kwamba wake kwa waume wote wanamkubali kwa uzuri huo na hata wote kumtamani.


 Hata hivyo hapo hapo kuna wale ambao huwa ni wazuri kawaida – ila kwa mtazamowake hujiona ni mzuri mno hakuna mfano kama yeye; kitendo ambacho kwa wachache kwenye kundi hili hufanya kujiona yeye ni yeye na kuwa kwa yeyote kuwa na yeye huyo mtu anatakiwa atambue kuwa ana bahati sana. 


Kitendo hiki hukuza nyodo za hali ya juu ya mwanamke mwenye mtazamo huu, kiasi kwamba wanapojitokeza wanaume kutaka kuoa – anaweza onyesha tabia kama maringo, dharau na kiburi.

 

Kujiona ana Umri mdogo

 

Binti yeyote wa miaka 18 na kuendelea anaruhusiwa kuolewa endapo tu karidhia kuolewa.


 Wanawake wametofautiana mipangilio yao ya kimaisha, kuna wale akiwa katika umri wa kuolewa hutamani sana kuolewa na kuna wale ambao hupenda kuolewa wakiwa wakubwa zaidi.


 Katika kundi hili umri kuwa mdogo hutegemeana, kuna mwingine anakuwa na umri wa miaka 25 na bado akajiona mdogo na hali kuna mwingine anakuwa na miaka 20 na akajiona ni mkubwa na anafaa kuolewa. 


Hii pia ni kwa wanawake wale ambao huwa na malengo ya kutotaka kuharakisha katika ndoa.


 Anapokuwa na umri ambao anaweza kuolewa lakini yeye hayupo tayari kwa muda huo, huwa ni kikwazo kwake kuingia katika ndoa.

 

Maradhi hasa UKIMWI

 

Hili kama lilivyo kwa wanaume -  Pamoja na kuhamasishwa kwingi na wataalamu wa maradhi ya HIV/AIDS kuwa mtu hata ukiwa umeathirika unaweza kuwa na mahusiano na hata kuoa na kuwa na watoto; bado haisaidii sana kwa vijana wanaojitambua kuwa ni waathirika wakiwa bado ni wadogo, hawajaoa/olewa ama kuwahi kuwa na mtoto. 


 Wengi sana hukata tamaa na huona ni kheri kubaki walivyo kuliko kuingia katika ndoa, hasa tokana na imani kuwa wanawake wakizaa wakati ni waathirika; afya hudhoofika zaidi.

 

Kutaka maisha ya Tamthilia (Ndoa za kuishi kwa furaha milele)

 

Kutokana na kukua kwa idadi ya tamthilia nyingi ambazo huonyesha maisha ya kimagharibi zaidi; kumekuwa na dhana kwa baadhi ya wanawake kutaka hayo maisha ya tamthilia yawe na kwao pia.


Hilo linafanya vigezo ambavyo mwanamke huyo anatumia kuchagua ama kukubali mwanaume kumuoa kutotimiza yale ambayo yeye binafsi anatarajia.  


Wengi hushindwa kutambua kuwa hakuna maisha ya furaha milele, na hasa kuwa maisha ya maigizo yapaswa kuchanganya na zako kuweza kufanya maamuzi ya kipi kiigwe na kipi kiachwe kama kilivyo.

 

Kuona taasisi ya Ndoa kama Utumwa

Mtazamo huu kwa wanawake wenye msimamo huu, huchangiwa na baadhi kama haya:

 

Usomi: Aina ya usomi ambao hupelekea kwa baadhi kuwa na tafsiri tofauti juu ya ndoa, haki, majukumu na mengine mengi.

 

Kushuhudia ndoa mbovu: Hii inaweza kuwa ya wazazi/walezi wake wenyewe (pengine mama aliteswa sana), na hata ndugu wa karibu kama vile kushuhudia kila ndoa ya ndugu yake anayoijua mwanamke huishi kwa mateso, manyanyaso na maisha ya taabu na kuonewa.

 

- Kuwa na uwezo sana wa kujitosheleza ambao unaweza kumtimizia na kufanya lolote lile ambalo anataka katika maisha. Kwake kuwa na mwanaume kama mume kwake anaona kama ni utumwa.

 

Kutokuwa kabisa na mshipa wa hisia za kufanya mapenzi

 

Kuna wanawake wale wachache waliozaliwa hivyo. Hawana hisia yoyote ile ya kimwili ya kuweza kupata hisia za kuweza kujisikia ama kutamani kufanya mapenzi. 


Wengi wa aina hii ya wanawake huwa ni waoga sana wa kuwa karibu na mwanaume, na kwa wale ambao wamewahi hata jaribu baadhi huona kama kitendo cha ndoa ni kero, unyanyasaji na uchafu.  


 Hivyo wazo la kuwa akiolewa anatarajia kufanya kitendo cha ndoa mara kwa mara kinamvunja kabisa hamu ya kutaka kuolewa.

Tuesday, October 29, 2013

RAY C ANARUDI KWA VISHINDO AMPA KIPIGO CHA MWAKA NORA


Na Musa Mateja

KATIKA hali ya kushangaza, siku chache baada ya kuripotiwa kupona na kuacha matumizi ya madawa ya kulevya, mwanamuziki Rehema Chalamila ‘Ray C’ anadaiwa kugeuka mwanamasumbwi na kumpa kipigo mwigizaji Nuru Nassoro ‘Nora’, Ijumaa Wikienda limenyetishiwa.

Kwa mujibu wa shuhuda wetu, tukio hilo lilijiri wiki iliyopita ndani ya studio moja ya kurekodia muziki iliyopo Kinondoni, Dar ambapo wawili hao walikutana walipokwenda kurekodi ngoma zao.
Ilidaiwa kuwa akiwa studio hapo, Nora alikutana na Ray C ambaye pia alizama mahali hapo bila mawasiliano na prodyuza anayemtengenezea ngoma mpya.


Chanzo hicho kilipasha kuwa baada ya Ray C kuingia studio hapo alimkuta prodyuza huyo akiandaa ngoma ya Nora ambapo alihoji kilichompeleka mwigizaji huyo mahali hapo.

Ilidaiwa kuwa prodyuza huyo ambaye jina halikupatikana alimwambia Ray C kuwa Nora alifika kurekodi wimbo wake.

Ilisemekana kuwa Ray C hakuridhishwa na majibu hayo, akaomba asikilizishwe ngoma hiyo ya Nora lakini baada ya kusikiliza ilidaiwa kwamba Ray C aliiponda mbele ya Nora, jambo ambalo mwigizaji huyo hakufurahishwa nalo.
Ilidaiwa kuwa Nora alipandwa hasira na kujikuta akimjibu mbovu Ray C.

Habari ziliendelea kutiririka kuwa siku hiyo walimalizana kwa kusonyana na siku iliyofuta walikutana tena studio hapo ambapo Ray C alidaiwa kutinga akiwa ‘masanga’.
Ilisemekana kuwa alipomuona Nora alianza kumpa vijembe, jambo lililosababisha Nora kushikwa hasira ndipo wakavaana na kuzichapa.

Hata hivyo, ilidaiwa kuwa Ray C ndiye aliyeibuka bingwa wa ndondi hizo kwa kumtwanga Nora hadi kumvimbisha jicho kabla ya maprodyuza na watu wengine kufanya kazi ya ziada kuwaamulia.
Ilisemekana kuwa baadaye Ray C alitolewa nje ndipo akahamishia hasira kwenye gari la Nora aina ya Toyota Vitz kisha akalivunja kioo na kutambaa zake.

Baada ya kupenyezewa ‘niuz’ hizo gazeti hili lilimtafuta Nora ambaye alikiri kutokea kwa sekeseke hilo huku akibainisha namna alivyoumizwa jicho lake na kuvunjiwa kioo cha pembeni cha gari lake.
Aliongeza kuwa siku hiyo alipoteza pochi wakati wa ugovi huo.

“Ray C alinikuta studio nikifanya wimbo, kilichonishangaza baada ya kuniona tu alibadilika ghafla.
“Nilijua angenishauri kwa kuwa ndiyo ninaanza gemu kumbe mwenzangu alifikiria vingine,” alisema Nora na kuongeza:
“Mbali na kuniumiza jicho lakini alinifanyia mambo ya ajabu sana, kama kusingekuwa na watu wa kutuamulia basi chochote kingetokea.

“Sikwenda kuripoti polisi. Niliamua kusamehe kwa sababu kuna watu walinisihi niachane naye kwa sababu bado kuna mambo yanamwendesha. 

Kwa upande wake Ray C alitafutwa kwa kila njia kupitia simu ya mkononi na kumvizia studio lakini hakupatikana hivyo juhudi za kumpata zinaendelea.

BABA DIAMOND ACHEKELEA MWANAYE KUMRUDIA WEMA


Na Gadness Mallya

Baba mzazi wa staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’, Abdul Jumaa amejikuta akiangua kicheko ‘hevi’ baada ya kusikia taarifa za mwanaye kurudiana na aliyekuwa zilipendwa wake, Wema Isaac Sepetu.

Akizungumza na mwanahabari wetu juzikati, Baba Diamond alisema alifurahishwa mno na hatua ya mwanaye kurudiana na Wema kwani ndiye mwanamke anayejielewa na ana nyota kali tofauti na warembo wengine aliowahi kuwa nao.

“Wema ni mwanamke mwenye nyota kali sana na anapendwa na wengi. Siyo kama hao akina sijui Penny (Penniel Mungilwa).


“Hana majivuno hata mimi nilisema mwanzoni walipoachana kuwa Diamond alipoteza bahati lakini sasa naamini atafika mbali zaidi kwani kama siyo kuachana kwao, Diamond angekuwa mbali,” alisema.


Hata hivyo, alimtaka Diamond kutulia na Wema kwani ndiye mwanamke sahihi kwake na aepuke kutangatanga kwani atashindwa kufanya mambo ya maana yatakayomuwezesha kuwa juu zaidi ya hapo alipo kwa sasa.


Hivi karibuni Diamond alithibitisha kurudiana na Wema wakiwa China lakini alipotua Bongo akaendelea na uhusiano wake na Penny hivyo kuwaacha mashabiki wake njiapanda

SINTAH AMCHANA AUNTY LULU LIVE KWA KUGAWA URODA BURE KWA MIDUME.


Katika mahojiano yake na gazeti moja hapa jijini nimesikia aunt lulu akisema wanaume wamemla sana uroda bure kwa miaka mingi sana bila faida, ila kwa sasa harudii kosa hilo ni mwendo wa faranga kwa kwenda mbele, sincerely kwa hizo pics hapo juu nani anaweza akawa na mwanamke kama huyu and shower her dollazzzz?? men also haaaaa as they say one man's meat is another man's poison.

 kwahio tusiliongelee sana ila wakati mwingine maneno tunayaongea ktk media yanafanya wasanii waonekane kituko katika jamii kabisa na akili zako na unajitambua wewe ni msanii  unaweza ukaongea pumbaless kama hii na watu wakasoma na kukuelewa ??

WANAUME WAMENILA URODA BURE MIAKA MINGI SANA BILA FAIDA SASA HIVI SIRUDII KOSA NG'OO: ANT LULU!

hiki ni nini wajameni? nikisema mtasema Sintah anaongea?? niko hapa kwaajili ya kurekebisha watu na jamii inachukulia wasanii kama kioo chao, sasa kwa matendo haya ya lulu na alivyoongea wengine tunaonekana vipi,

ni wakati umefika sasa tujue kuna wasanii na wanaotafuta umaarufu ili ya kwao yawaendee eg kupata mabwana na wanawake 

yaani nimekereka sana na hii kauli ya Aunt Lulu so sasa hivi anauza rasmi na ameamua kujitangaza kama tunavyojua biashara ni matangazo ?? God  forbid.


i do the seeking n u do the judging...

NEY WA MITEGO AKAIDI AMRI YA BASATA YA KUTOKUVAA MLEGEZO..AWAONYESHA USO WA MBUZI FIESTA


Msanii wa Hip pop Ney wa mitego 'TRUE BOY' Amewaonyesha uso wa mbuzi Basata ambao awali walimwonya kutokana na tabia yake ya kuvaa mlegezo "KATA K" akiwa jukwaani kwa madai ya kuidhalilisha sanaa hiyo..

Katika hali ya kushangaza kabisa Msanii huyo ameonekana kupuuzia agizo hilo la basata na kendelea kuvaa mlegezo wakati akilishambulia Jukwaa huku akishangiliwa na mashabiki lukuki wa Bongo Fleva .


Tukio hilo lilitokea jana wakati wa Show ya FIESTA DAY 2 iliyofanyika kwenye viwanja vya Leaderz Club alipokuwa akiwapagawisha wapenzi wake na kibao chake cha "MUZIKI GANI" Akiwa sambamba na Msanii mwenzake Diamond Platinumz.

Sasa wapenzi wa Bongo fleva wanasubiri Rungu la Basata liweze kufanya kazi yake huku wengi wakionekana kumtetea kwa kudai kuwa kila mtu ana aina ya maisha yake 'Life Style'

BEN POL AIMISS M-LAB STUDIO ATAJA FAIDA NA HASARA ZA KUONDOKA LABEL HIYO


Ben Pol amezielezea faida na hasara za kuondoka kwenye label iliyomtambulisha, MLab huku akisema kwa sasa hana uhuru wa kurekodi nyimbo nyingi kwa wiki kama alivyokuwa kwenye label hiyo.


“Sasa hivi sina freedom ya kurekodi nyimbo 3 kwa wiki kwasababu itabidi upige simu, ufanye booking hata two weeks before, uende utengeneze beat, unaweza ukarekodi wimbo mmoja miezi miwili au mwezi mmoja. Lakini kipindi nipo MLab unarekodi nyimbo nne, hizi Maneno, Nikikupata, Maumivu, ndani ya wiki moja nimerekodi nyimbo tatu kwasababu una all access ya studio, unaweza ukarekodi hata nyimbo mbili siku moja, yaani hiyo access ndio nimeimiss sasa hivi,” alisema Ben Pol.


Akizungumzia faida za kuondoka MLab, Ben Pol amesema kwa sasa ana meneja wake binafsi ambaye ni kaka yake na hivyo mazingira ya kufanya kazi ni rahisi tofauti na kuwa chini ya uongozi wa label.


“Kunakuwa na mlolongo mkubwa hata kama ikitokea kazi kuona maslahi yake ni adimu sana tofauti na ukiwa unafanya mwenyewe.”