AMANDA APIMA NGOMA, PRESHA YAPANDA YASHUKA
MSANII wa filamu za Kibongo, Tamrina Poshi ‘Amanda’ hivi karibuni
alijikuta akipandwa na kushukwa na presha mara baada ya kwenda
hospitali kupimwa Ugonjwa wa Ukimwi.
Kikizungumza na Exclusive chanzo makini ambacho kilishuhudia tukio zima
katika Hospitali ya Dokta Mvungi, Kinondoni, jijini Dar kilisema baada
ya Amanda kupewa majibu ya vipimo na daktari, alianza kuhaha huku na
kule kama mtu aliyechanganyikiwa, kisha presha ikampanda baadaye
ikashuka.…
MSANII wa filamu za Kibongo, Tamrina Poshi ‘Amanda’ hivi karibuni
alijikuta akipandwa na kushukwa na presha mara baada ya kwenda
hospitali kupimwa Ugonjwa wa Ukimwi.
Kikizungumza
na Exclusive chanzo makini ambacho kilishuhudia tukio zima katika
Hospitali ya Dokta Mvungi, Kinondoni, jijini Dar kilisema baada ya
Amanda kupewa majibu ya vipimo na daktari, alianza kuhaha huku na kule
kama mtu aliyechanganyikiwa, kisha presha ikampanda baadaye ikashuka.
Baada ya kuzinyaka habari hizo, paparazi wetu alimtafuta Amanda na kumuuliza juu ya tukio hilo ambapo bila hiyana alitiririka:
“Ile
ilikuwa ni mara ya tatu kupima ngoma yaani wakati nikisubiri majibu,
presha ilipanda ghafla mpaka daktari akawa na wakati mgumu wa kunipa
majibu.
“Nilienda
kuchukua majibu na sikutaka kuyaangalia, nilimpelekea daktari ambaye
aliniambia niko safi yaani sikuamini nilitoka nikiwa naongea peke yangu,
nilikuwa sijiamini si unajua tena ujana ni maji ya moto sasa presha ,”
alisema Amanda.
No comments:
Post a Comment