POOL PARTY

POOL PARTY

Tuesday, July 16, 2013

Ney wa Mitego, baada ya ujauzito wa GF wake kutoka: Namuachia Mwenyezi Mungu, tutajaaliwa mwingine nafkiri may be ndio itakuwa rizki yetu.


Girlfiend wa Rapper Ney wa Mitego "Siwema" ambae alikuwa na ujauzito wa Rapper huyo, bad news ni kuwa mimba hiyo imetoka mara baada ya kuanguka akiwa bafuni baada ya kusikia kizunguzungu. Ney wa Mitego ameeleza kisa kilivyotokea.

"Alianguka nini bahati mbaya ndio kama hivyo, namuachia mwenyezi mungu, tutajaaliwa mwingine nafkiri may be ndio itakuwa rizki yetu.
Ilikuwa ijumaa mida ya mchana mchana, alikuwa kazini akasema kichwa kama kinamuuma hivi,akaniambia bana mi natoka hapa sijiskii vizuri acha nirudi home, alivyorudi home akawa ameingia kuoga, alivyoingia kuoga aakajiskia kizungu zungu akadondoka bafuni, akawa amepoteza fahamu kama siku nzima, kwahiyo mwisho wa siku nikawa naongea na Dr, akawa anafight katika juhudi zake zote kasema hapa lazima tuokoe kimoja, kwahiyo tuangalie tufanye nini, tufanya maamuzi ya kitu uzima, kwahiyo tukajua, tukasema no way out inabidi tu afanye tu anachokiweza yeyey Dr." amesema Ney wa Mitego.

No comments:

Post a Comment