POOL PARTY

POOL PARTY

Wednesday, December 17, 2014

Young Suma na GNako waja na collabo


Msanii wa muziki wa bongo flava nchini Tanzania, Young Suma anatarajia kuachia audio ya wimbo wake mpya unaoitwa ‘Hatujivungi’ aliomshirikisha Mfalme wa viitikio ambaye pia ni rapa kutoka kundi kali la muziki lenye makazi yake jijini Arusha, G-Nako hivi karibuni.

Young Suma ameiambia hivisasa blog kuwa wimbo huo utakuwa ni zawadi maalumu kwa mashabiki na wapenzi wa muziki wake hasa katika msimu huu wa sikukuu.

Wimbo ‘Hatujivungi’ umetayarishwa na mtayarishaji mahili nchini, Levybeat ambapo, Young Suma amesema kazi hiyo ni ya kipekee kutokana na style ya kurap na kuimba iliyoitumika pamoja na beat ilivyo kali.

No comments:

Post a Comment