POOL PARTY

POOL PARTY

Wednesday, June 19, 2013

OMMY DIMPOZ AOMBA MSAMAHA

Na Mwandishi Wetu

KUFUATIA kumtusi marehemu Albert Mangweha ‘Ngwea’ kuwa amekufa maskini, mmiliki wa akaunti inayodaiwa ni ya msanii Omary Faraji Nyembo ‘Ommy Dimpoz’ katika mtandao wa Facebook, amewaomba msamaha Watanzania kwa kitendo chake hicho baada ya kumwagiwa mitusi.

Omary Faraji Nyembo ‘Ommy Dimpoz’.
Katika akaunti hiyo yenye jina la Ommy Dimpoz- Omary Faraji, mwishoni mwa wiki iliyopita ilijaa matusi na maneno makali yakimnanga jamaa huyo kwa kauli yake aliyoitoa hivi karibuni kwenye Tuzo za…
Na Mwandishi Wetu
KUFUATIA kumtusi marehemu Albert Mangweha ‘Ngwea’ kuwa amekufa maskini, mmiliki wa akaunti inayodaiwa ni ya msanii Omary Faraji Nyembo ‘Ommy Dimpoz’ katika mtandao wa Facebook, amewaomba msamaha Watanzania kwa kitendo chake hicho baada ya kumwagiwa mitusi.

Omary Faraji Nyembo ‘Ommy Dimpoz’.
Katika akaunti hiyo yenye jina la Ommy Dimpoz- Omary Faraji, mwishoni mwa wiki iliyopita ilijaa matusi na maneno makali yakimnanga jamaa huyo kwa kauli yake aliyoitoa hivi karibuni kwenye Tuzo za Kili.
Aliandika: “Binadamu ni kukosea mara nyingi na-regret (kujuta) kwa yale niliyosema kuhusu Ngwea. Kama ningekuwa na uwezo wa kurudisha siku na maneno nyuma, yale ndo yangekuwa ya kwanza.
“Nakubali nilifanya kosa kubwa sana na nikaweka pride (majivuno) yangu na sifa zangu mbele bila kufikiria nitakayosema.
“Nyumbani Tanzania, Bongo nimeenda hadi kwa redio stations kuwaomba msamaha.

Albert Mangweha ‘Ngwea’.
“Team Kigoma All Stars na wasanii wenzangu wa Bongo, Kenya, Uganda na nchi nyingine zote nisameheni tafadhali.
“I have learnt to think about what I say before I Talk or let it out of my mouth (Nimejifunza kufikiri chakusema kabla ya kukizungumza au kukiacha kitoke mdomoni mwangu).
“Nimewakosea familia ya Ngwea na ma-fans (mashabiki) wangu wanaonipenda hata pia kwa Allah Mungu Baba, naombeni msamaha tafadhali.”
Pamoja na kuomba msamaha bado watu waliendelea kumponda wakihoji ni kitu gani Ngwea alimfanyia huku mwanamuziki Khaleed Mohamed ‘TID Mnyama’ akiahidi kumpa kichapo.Baada ya kuomba msamaha, msanii huyo anayechipukia alidaiwa kupanga safari ya kwenda Morogoro kuiomba msamaha familia ya Ngwea.

No comments:

Post a Comment