POOL PARTY

POOL PARTY

Friday, June 21, 2013

DEMU WA MTU AMVAA TUNDAMAN JUKWAANI

Na Dustan Shekidele, Morogoro

MSANII wa Bongo Fleva, Khalid Ramadhan ‘Tundaman’ Jumamosi iliyopita alivamiwa jukwaani na demu wa mtu wakati akitoa burudani kwenye shindano la kumsaka Redd’s Miss Morogoro 2013 ndani ya Ukumbi wa Hoteli ya Kitalii ya Nashera mjini humo.

Tundaman aliyepanda jukwaani saa 7 usiku akiwa amechelewa na kusababisha kukorofishana na MC wa shoo hiyo kutokana na kuendelea kutumbuiza hata pale muda wake ulipokuwa umekwisha.

Hata hivyo, mzuka ulikuwa umewapanda mashabiki pamoja na Tundaman na kulazimika msanii huyo kushuka jukwaani na kuanza kucheza na mashabiki wake.

Tundaman ambaye alionekana kuchangamka kama vile alikuwa ‘ameonja,’ alirudishwa jukwaani na mabaunsa wake  kutokana na kuhofia usalama wake kutoka kwa mashabiki hao.

Akiwa jukwaani ndipo…

MSANII wa Bongo Fleva, Khalid Ramadhan ‘Tundaman’ Jumamosi iliyopita alivamiwa jukwaani na demu wa mtu wakati akitoa burudani kwenye shindano la kumsaka Redd’s Miss Morogoro 2013 ndani ya Ukumbi wa Hoteli ya Kitalii ya Nashera mjini humo.
Tundaman aliyepanda jukwaani saa 7 usiku akiwa amechelewa na kusababisha kukorofishana na MC wa shoo hiyo kutokana na kuendelea kutumbuiza hata pale muda wake ulipokuwa umekwisha.
Hata hivyo, mzuka ulikuwa umewapanda mashabiki pamoja na Tundaman na kulazimika msanii huyo kushuka jukwaani na kuanza kucheza na mashabiki wake.
Tundaman ambaye alionekana kuchangamka kama vile alikuwa ‘ameonja,’ alirudishwa jukwaani na mabaunsa wake  kutokana na kuhofia usalama wake kutoka kwa mashabiki hao.
Akiwa jukwaani ndipo alipovamiwa na demu huyo wa mtu aliyekuwa amevaa nusu utupu na kuanza kucheza naye kwa staili mbalimbali tukio lililowafanya watu kulipuka kwa shangwe huku mgeni rasmi, Mbunge wa Kilosa, Mustafa Mkulo naye akiwa hana mbavu.
Wakati Tundaman akiendelea kucheza na demu huyo, ghafla watu wote walishangaa kumuona demu huyo akimsukuma msanii huyo na kumwangusha chini kama gunia.
Aidha, demu huyo aliendelea kuwashangaza watu baada ya kumwangukia msanii huyo juu, ndipo wengine wakashtuka na kwenda kumsaidia Tundaman huku baadhi wakiendelea kucheka.
Mabaunsa na madansa wa msanii huyo ndiyo walikwenda kumpa msaada kwa kumwinua huku demu huyo naye akishika ustaarabu wa kurudi sehemu aliyokuwa ameketi awali.
Baada ya mrembo huyo kurudi sehemu yake, alikutana na kimbembe kwa kupewa kichapo kutoka kwa mtu wake ambaye alikuwa ametinga naye katika shoo hiyo.

No comments:

Post a Comment