POOL PARTY

POOL PARTY

Tuesday, October 15, 2013

SHAHIDI AELEZEA JINSI UFOO SARO ALIVYOPIGWA RISASI NA MAMA YAKE KUUWAWA


Kwa mujibu wa ITV tukio lilitokea saa kumi na mbili na nusu nyumbani alipokua akiishi mama mzazi wa mwandishi wa ITV Ufoo ambae ni Anastazia ambapo baada ya taarifa kufika ITV, timu ya ITV  ilifatilia tukio hilo na kushuhudia gari la wagonjwa la Hospitali ya Tumbi Kibaha Pwani ikiwa imembeba Ufoo kumuondoa kwenye hospitali hiyo ili kumuwaisha Muhimbili hospital.

Wakati huo mpaka Ufoo anafikishwa hospitali ya Muhimbili kwenye kitengo cha dharura, miili miwili ambayo ni wa mama yake mzazi na mwanaume aliemuua mama kwa risasi na kisha kujiua yeye pia kwa risasi ya kichwa ilikua ikiingizwa kuhifadhiwa.

Shuhuda wa tukio hilo ambae ni mpangaji aliepanga nyumba ya mama yake na Ufoo, Mr Ngowi amesema ‘walikua wanagombana huko ndani na kelele za bastola zinasikika, tukafika tukakuta damu zimetapakaa chini barazani tukamuona na mama amelala chini ndio nikatoa taarifa kituo cha polisi na kukuta Marehemu amemuua mama mkwe na yeye mwenyewe kujiua’


Mwenyekiti mtendaji wa IPP Reginald Mengi alifika hospitali kumjulia hali Ufoo ambapo alisema ‘nimesema na Madaktari ana majeraha lakini hatujui ni mangapi kwa sababu bado wanamfanyia uchunguzi na baadae kidogo atafanyiwa upasuaji, nina imani kwamba Ufoo atarudi kwenye hali yake ya afya njema’

No comments:

Post a Comment