POOL PARTY

POOL PARTY

Saturday, October 26, 2013

AMANDA:SIWEZI KURUDIA MATAPISHI HATA SIKU MOJA


Stori: Gladness Mallya

STAA wa sinema za Kibongo, Tamrina Poshi  ‘Amanda’ amefunguka kuwa hawezi kurudia matapishi yake kwa kurudiana na aliyekuwa mpenzi wake, Joseph Rashau ‘Bwana Misosi’.

Akichonga na paparazi wetu muda mchache baada ya wadau kibao kumtaka mwanadada huyo arudiane na mpenzi wake huyo kupitia mtandao wa kijamii wa Facebook, Amanda alisema tayari ameshapenda kwingine hivyo hapendi kumzungumzia mtu aliyeachana naye pia hana tabia ya kurudia matapishi yake.


“Siwezi kurudiana na Misosi kwani nikishaachana na mtu basi ninamtoa moyoni mpaka mdomoni nikiwa na maana sina muda wa kukaa na kumzungumzia ndiyo maana hata wadau waliokuwa wakinitaka nirudiane naye sijawajibu chochote,”alisema Amanda.

No comments:

Post a Comment