POOL PARTY

POOL PARTY

Friday, October 11, 2013

PRODUCER HAMMY B ARUDISHWA TENA TUSKER PROJECT FAME BAADA YA ALLI ZORRO KUTEMWA


MTAYARISHAJI mahiri wa muziki wa Kizazi kipya, anayemiliki studio za ya B Hits, Hermes Bariki ‘Hermy B’ ameteuliwa kuwa Jaji wa shindano la kusaka vipaji vya kuimba Afrika Mashariki la Tusker Project Fame.

Mkali huyo anayemiliki studio za B Hits, ataiwakilisha Tanzania na kwa kuungana na majaji wengine jijini Nairobi, nchini Kenya akichukua nafasi ya Zahir Zorro aliyekuwa Jaji katika shughuli ya kusimamia usaili wa shindano hilo.

Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Meneja wa bia ya Tusker, Sialouise Shayo, alisema katika kuelekea awamu ya kwanza ya shindano hilo msimu huu wa sita, wamejipanga kuhakikisha Watanzania wanahusishwa kikamilifu.

“Kama tunavyomkaribisha Jaji mpya Hermy B ambaye amekuwa katika kinyang’nyiro hiki cha Tusker Project Fame kwa muda mrefu, tunatumia fursa hii kuwatangazia Watanzania kuwa tumejifunza mengi kupitia kwa Zorro,” alisema.

Katika shindano hilo, Tanzania inawakilishwa na Angela Karashani, Elisha Simon, Mgeni Kalinga na Ussa Dubart.

Kwa upande wake, Hermy B aliishukuru Tusker kwa kumchagua kuwa Jaji katika shindano hilo kwa mara ya sita pamoja na Zahir Zorro.


Mshindi wa Tusker Project Fame atajinyakulia Sh 100, 000, 000 na mkataba wa kurekodi utakaogharimu Sh 200, 000, 000.
-Mtanzania

No comments:

Post a Comment