POOL PARTY

POOL PARTY

Saturday, June 7, 2014

Hivi Huyu Halima Kimwana ni Nani Kwa Diamond?

Kuna watu wanashangaza kidogo,siyo kwamba tunawafuata majumbani mwao na kugundua tabia zao,kwamba wanakula sana,wachoyo,wachafu au hawapatani na majirani zao,hapana,wanayoyafanya ama kuzungumza,wanatufanya tuwatambue.Lakini tunaishia kuwajua kwa majina na matukio yao.Ukiniuliza babu Tale ni nani,fasta nitakujibu kuwa ni msaidizi wa shughuli za Diamond,Romie Jones nitakuambia ni ndugu yake Diamond,Wema Sepetu,ni usingizi wa Diamond,kwa maana ya mpenzi,lakini ukiniuliza Halima Kimwana ni nani,naweza kulipuuzia swali lako kwa maana sitambui wala kujua ni nani kwa Diamond.
Siwezi kuacha kujiuliza hivi huyu binti wa mjini  ni nani kwa Diamond?rafiki,dada,shemeji yake,mpambe au nani,Au ndiye kiunganishi chake kwa wale viumbe waliosababisha aitwe sukari ya warembo?yeye ni nani haswa hata afikie hatua ya kumchagulia Diamond mpenzi wa kuwa nae,ni nani hasa hata afikie kumaindi uwepo wa Wema kwenye himaya ya Diamond,kajina kake kamezidi kukaa on ea kwa kipindi kirefu kutokana na uwepo wake karibu na Diamond,ana nguvu sana kwa Diamond,Nilipuuzia kwa muda mrefu sana nikiamini ni mtu wake wa karibu wa kumshikia poda awapo lokesheni ya video zake,au anashikilia simu zake awapo stejini,baadae nikadhani kuwa huenda ni msaidizi wa mambo binafsi ya Diamond.Lakini kufikia hatua ya kumpangia Diamond mwanamke  wa kuwa nae,kidogo hapo nashindwa kuelewa,yeye ni nani kwa Diamond?
Wadau mnaojua uhusiano wa huyu dada hebu mtujuze,ni nani,anafanya shuhuli gani,naamini wote mliosoma gazeti hilo mna kiu ya kujua.
Source:Gazeti la KIU ya jibu toleo no 1275 la tarehe 2-5/6/2014 
Via Sintah Blog

Jeshi la Polisi Linadaiwa Kuvamia Nyumbani kwa Lwakatare na Kuwakamata

Taarifa ya awali...
Katika hali ile ile ya mwendelezo wa kutumikia maelekezo na maslahi ya CCM dhidi ya wapinzani wa kisiasa wa chama hicho, Jeshi la Polisi usiku huu limevamia nyumbani kwa Mkurugenzi wa Ulinzi na Usalama wa CHADEMA, Wilfred Lwakatare na kumkamata housegirl wake.
Kama hiyo haitoshi, jeshi hilo la polisi limewakamata wafanyakazi wengine wawili (house boys) wa Lwakatare. Hadi muda mfupi uliopita vijana hao wawili, walikuwa wako Kituo cha Polisi Mbezi huku msichana wa kazi wakizunguka naye kwenye gari la patrol bila kumfikisha kituoni.
Jeshi hilo la polisi kupitia kituo hicho cha Mbezi lilikuwa linawatisha kila mtu anayekwenda hapo kituoni kuulizia sababu za vijana hao kukamatwa, lakini hatimaye mmoja wa watu walioko kituoni hapo ametonya kuwa polisi wanasema mmoja wa vijana hao kesi yake iko Arusha!
Kijana anayetaka kubambikiwa kesi huko Arusha ni mwanagenzi kabisa mjini. Hata ukimwambia aende Chalinze au Wami hawezi kupajua. 
Hatimaye mbinu za CCM kupitia jeshi la polisi ya kutaka kukichafua CHADEMA au viongozi wake kwa kutumia kes za kubambikia ugaidi imerejea tena...
Tutawaletea taarifa kamili...
JF

Thursday, June 5, 2014

Mmiliki wa nyimbo za Bob Marley aamuliwa...

Bob Marley
Mzozo wa kisheria juu ya nani anayemiliki baadhi ya nyimbo maarufu za reggae duniani umemalizika mjini London.
Nyimbo hizo zilizotungwa na kuimbwa na msanii Bob Marley zimekuwa ziking'ang'aniwa na kampuni 2 pinzani juu ya umiliki wao.
Jaji katika mahakama kuu, Richard Meade alikata kesi ambapo kampuni ya Cayman Music ilikuwa inadai kumiliki nyimbo 13, miongoni mwao wimbo uliopata umaarufu 'No Woman, No Cry' kuwa haina haki nazo tena.
Kampuni hiyo ilikuwa imedai kuwa nyimbo hizo hazikujumuishwa walipouza baadhi ya haki zake kwa kampuni nyingine mnamo mwaka wa 1992.
Kampuni ya Cayman imesema kuwa Bob Marley aliandika nyimbo hizo chini ya majina tofauti, lakini Jaji ameamua kuwa bado kandarasi waliouzia inafunika nyimbo zote hizo.
Bob Marley alifariki mwaka wa 1981 baada ya kuugua maradhi ya saratani kwa muda.

WEMA,AUNTY NA SHILOLE WALIPULIWA BUNGENI KUWA NI VINARA WA KUVAA NGUO ZISIZO ZA MAADILI

 
Ukiukwaji wa maadili ni sehemu ya kilio cha jamii ya watanzania na tayari kilio hicho kimeifikia serikali ambayo imechukua hatua za awali ya kuwaonya watu wanaofanya tabia hizo.Naibu Waziri wa habari,Vijana, Utamaduni na Michezo Juma Nkamia ameeleza hatua ambazo wizara hiyo imechukua katika kukomesha ukiukwaji wa maadili unaofanywa hasa katika kumbi za starehe.Akijibu swali lililoulizwa na mbunge Catherine Magige, Nkamia amesema kuwa serikali imefanya vikao na wamiliki wa kumbi za starehe, wamiliki wa bendi, maafisa wa utamaduni, na wakuu wa polisi.
Amesema serikali imezuia kutoa vibali kwa vikundi vya ‘Kangamoko’ kutokana na uchezaji wake kutofuata maadili na kutoa mfano wa wasanii ambao wamepewa onyo.
“Mfano wasanii waliopewa onyo ni Nay wa Mitego, Shilole na Anti Ezekiel. Na kwa upande wa kumbi ni Mamas &Papas.” Amesema

Naibu waziri huyo ameeleza kuwa serikali imeunda kamati ya kitaifa yakuzuia ukatili, unyanyasaji wa watu wenye ulemavu wa ngozi na watoto na pia udhalilishaji wa wanawake.

UKIKUTANA NA MHESHIMIWA RAIS WA NCHI UTAMUELEZA SHIDA GANI?

Kwa upande wa Staa wa Bongo Fleva,Diamond Platnumz hivi karibuni alipoenda nchini Marekani alipata nafasi ya kukutana na rais wa jamhuri ya muungano wa tanzania,Dr Jakaya Mrisho Kikwete na alipoulizwa akamwambia shida yake ni kufanya kolabo na wasanii wakubwa, ambapo rais Kikwete alimkutanisha Diamond na mdau mkubwa wa muziki aliyewahi kuwa rais wa record label kubwa ya Def Jam, na makamu wa rais wa Island Def Jam.Mchana huu Diamond anatarajia kupaa kuelekea South Africa kwa ajili ya tuzo za MTV zinazotarajiwa kufanyika Jumamosi wiki hii, na alikua na haya ya kusema kwa mashabiki wake.

Aunt Lulu Alia Kukosa Bwana wa Kizungu kutoka Thailand

Na Hamida Hassan

MKALI wa sinema za Kibongo, Lulu Semagongo ‘Aunt Lulu’ amefunguka kuwa anasikitika kukosa bwana aliyeahidiwa na marehemu Amina Ngaluma.

Akizungumza na paparazi wetu, Aunt Lulu alisema kabla marehemu Amina hajapatwa na mauti nchini Thailand, alimuahidi kumtafutia bwana nchini humo lakini mauti yalimkuta kabla hajamtimizia ahadi hiyo.

“We acha tu, aliniahidi kunitafutia mume baada ya kugundua nasumbuliwa na wanaume kila wakati lakini ndiyo hivyo tena Mungu akamchukua kabla hajanitimizia ahadi,” alisema Aunt Lulu.
Amina alifariki mwezi uliopita nchini humo ambapo chanzo cha kifo chake kikielezwa kuwa ni uvimbe kwenye kichwa.

Huyu ndiye binti anayedai kubakwa na mume wa Flora Mbasha

Huyu Ndio Msichana Ambaye Anahusika na Sakata linaloongelewa sana la Mume wa Flora Mbasha Kumbaka Shemeji yake...Basi huyu Ndio Shemeji Mwenyewe Wajameni
Angalia muonekano wake utapata maswali mengi.